Mgogorowa uchumi duniani, mgogoro wa chakula duniani na tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa mambo haya yote yanaathirika kwa kiasi kikubwa watu wa duniani ambao wanakabiliwa na matokeo wa umaskini kwa shida zaidi kutokana na mazingira yao wanapoishi ni magumu sana.
Zaidi ya asimilia 30 za watu wanaoishi duniani ni wamaskini (watu bilioni 2,7 wanaishi na dola 2 kwa siku[1]). Mgogoro wa chakula duniani ikachangia hali mbaya iendelee, kutokana na watu mamilioni 925 wanakabiliwa na njaa. Kutokana na tatizo la uchumiwa duniani haja kubwa ni kupata aina ya uchumi ambao unazingatia utekelezaji wa haki za binadamu na uwe endelevu ndani ya jamii na duniani. Pia kutokana biashara inatakiwa wazalishaji na wakulima wadogo wadogo wapate maendeleo endelevu pamoja na nafasi za maendeleo.
Biashara inatakiwa ifaidike wale ambao wanaishi kwenye mazingira magumu. Biashara ina uwezo kusaidia watu.
Biashara ya Haki ni mkakati wenye ufanisiambao unasaidia kuondoa umaskini
Biashara ya Haki inachangia kujenga uchumi ambao mfumo wake unaheshimu haki za binadamu na kupata uchumi endelevu ndani ya jamii na duniani
Tarehe 14 mwezi wa tano mwaka 2011, wazalishaji, wafundi, wakulima na wenye viwanda vidogo mamilioni, pamoja na wazalishaji, wafanya biashara na walaji ambao wanafanya kazi ndani ya mfumo wa biashara ya haki, hawa wote wataadhimisha Siku ya Biashara ya Haki Duniani.
Jamii ya wafanyabiashara, ya walaji pamoja na watengenezaji wa sera, vyombo vya habari, maelfu ya miradi ya kijamii, mashirika yasiyo ya kiserikali na zaidi ya elfu mia moja ambao wanajitolea wote wanahimiza maadhimisho ya Siku ya Biashara ya Haki popote duniani.
Biashara ya Haki Duniani Mwaka 2011 mada yake ni “BIASHARA KWA WATU – Ufanye biashara ya haki na dunia yako”
Mada hiyo inazingatia umuhimu wa kuwekea watu na mazingira katikati ya mfumo wa biashara na wa haraja, Biashara kwa watu inamaanisha kwamba inaweza kuchangia maendeleo endelevu kwa jamii ujumla. Biashara ya Haki ikaanzishwa zaidi ya miaka 50 iliyopita, kw hiyo tunaweza kusema tumepata nafasi nyingi kuhakikisha kwamba Biashara Haki ni mkakati ambao unafaa sana kwa ajili ya kuondoa umaskini; biashara ina uwezo kubadilika na kuboresha maisha ya jamii.
Ufanye biashara ya haki na dunia yako mada hiyo inahusika wanunuaji binafsi wazingatie Biashara ya Haki huku wananunua bidhaa, inahusika wafanyabiashara wazingatie Biashara ya Haki huku wananunua stoo na kwa ajili ya ofisi zao, inahusika serikali za jamii na serikali za rai wazingatie Biashara ya Haki kwenye mipato wa umma kwa ajili ya kuhimiza wananchi wajue wajibu wao wakati wananunua.
Biashara ya Haki ni biashara nzuri kwa watu wote, toka wazalishaji mpaka wanunuaji.
Shirika la Kimataifa la Biashara ya Haki, mtandao wa dunia unaohusisha Mashirika ya Biashara ya Haki ndani ya nchi 73 popote duniani, linakuhimiza kushirikiana kwenye maadhimisho ya Siku ya Biashara ya Haki Duniani Mwaka 2011.
Utie saini azimio lile. Udhimishe Siku ya Biashara ya Haki Duniani. Wote pamoja tunaweza kufanya mabadiliko yafike.
SIGN THIS DECLARATION HERE!
By signing you accept our Privacy Policy.
Kwa kupata taarifa zaidi :
This e-mail address is being protected from spambots, you need JavaScript enabled to view it
www.WFTDay.info
____________________
Shirika la Kimataifa la Biashara ya Haki (WFTO) ni mtandao wa dunia unaohusisha Mashirika ya Biashara ya Haki popote duniani. Inawakilisha zaidi ya Mashirika ya Biashara Haki katika nchi 73 ambayo yanatokea Afrika, Asia, Amerika Kusini, Ulaya, Amerika Kaskazini na Pasifiki.
Lengo la Mashirika ya Biashara ya Haki ni kuwapa wazalishaji na wakulima wadogo wadogo nafasi za kuboresha maisha yao pamoja na jamii kutokana na utekelezaji wa Biashara ya Haki. Mashirika ya Biashara ya Haki ni mtandao wa dunia na yanatetea Biashara ya Haki kwa ajili ya kuhakikisha sauti za wazalishaji zisikilizwe.
[1]Zaidi ya watu bilioni moja wanaisihi na dollar moja kwa siku. Data: UN Millenium Project and FAO.
|